• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Temeke Municipal Council
Temeke Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Utawala na Utumishi
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Mazingira na Maji taka
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Tehama na Uhusiano
      • Ugavi na Ununuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Investment profile
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Watumishi
    • Ujasiliamali
  • Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipango miji na Mazingira
      • Kamati ya Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu mbalimbali
    • Mpango mkakati
    • Ripoti
      • Fomu ya maadili
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbalimbali
    • Social economic profile
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

MWAROBAINI UKUSANYAJI KODI ZA MAJENGO TEMEKE WAJA.

Posted on: February 3rd, 2021

Kufuatia muongozo mpya wa Serikali kuhusu ukusanyaji wa kodi za majengo,ushuru wa mabango na vitambulisho vya wajasiriamali kusimamiwa na Wakurugenzi wa halmashauri;uongozi wa manispaa ya Temeke umeanza kujiandaa kutekeleza agizo hilo.

Akiongea na waandishi wa Habari Mkurugenzi wa manispaa hiyo Bw.Lusubilo Mwakabibi alisema kuwa wameandaa utaratibu utakaowawezesha kutambua idadi kamili ya nyumba zilizopo kwenye Manispaa hiyo ili kuweza kufanikisha zoezi la ukusanyaji wa kodi hiyo ya majengo.

"Leo hii tarehe 3 mwezi huu wa pili nimeita watendaji wangu wote wa mtaa na kata tupange namna ya kwenda kukusanya mapato".Alisema Bw.Mwakabibi

Aidha Bw.Lusubilo alitoa maelekezo kwa watendaji wa mitaa na kata kuhakikisha zoezi hilo la utambuzi wa majengo linafanyika kwa wakati ili kurahisisha zoezi hilo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa watendaji wa kata wa wilaya ya Temeke Bw.Anzamen Mandari alisema baada ya kupata maagizo hayo ya Mkurugenzi,watahakikisha hakuna nyumba au jengo litakaloachwa bila kulipa kodi.

Naye Afisa mtendaji wa kata ya Buza Bi Hulda Ulomi alimpongeza Mh.Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuweka msisitizo katika suala zima la ulipaji wa kodi ambazo ndizo zinasaidia kufanya miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

"Tumekuja hapa kupata maelekezo na tutahakikisha kuwa haya tuliyoelekezwa leo tunayafanyia kazi".Alibainisha Bi Mtendaji huyo.

Februari mosi mwaka 2021 Serikali kupitia Waziri Ofisi  ya Rais Tawala za Mikoa na Serikalu za Mitaa Mh.Suleimani Jafo alitoa muongozo mpya wa serikali juu ya ukusanyaji wa kodi mbalimbali kurudishwa chini ya wakurugenzi wa Halmashauri Nchini.


Baadhi ya watendaji wa Kata na Mitaa wakiwa katika kikao kazi ukumbi wa Manispaa Iddy Nyundo mapema leo

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA AWAMU YA PILI KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA TEMEKE 2021 January 08, 2021
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA WA MASOMO 2021 December 15, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA WILAYA YA TEMEKE MWAKA 2021 December 18, 2020
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI November 16, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI TEMEKE AKABIDHIWA MAGARI NANE (8) YA KUZOLEA TAKA.

    March 03, 2021
  • MAMA SAMIA AWAHAKIKISHIA NEEMA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WAKUBWA.

    February 14, 2021
  • DC TEMEKE ATOA SIKU 14 KWA MZABUNI WA VIFAA TIBA KITUO CHA AFYA BUZA

    February 12, 2021
  • DC GONDWE AGEUKA "MBOGO" KWA MKANDARASI DART.

    February 08, 2021
  • Angalia zote

Video

TEMEKE YA VIWANGO
Picha jongefu za ziada

Kurasa za Karibu

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - 2019
  • Vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Salary Slip Portal
  • Email za watumishi wa serikali TemekeMC (GMS)
  • National WASH Data Platform

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • Tovuti ya Taifa
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
  • Utumishi
  • Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Manispaa ya Temeke inapatikana mkabala na uwanja wa Taifa katika makutano ya barabara ya Mandela na Taifa.

    Anuani ya Posta: P.O.Box 46343 Dar-es-Salaam

    Simu ya Mezani: +255 22-2928132

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: temeke@temekemc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Mtandao

Hatimiliki©2018. Halmashauri ya Manipaa ya Temeke